Hakuna ubishi kuwa mwaka 2016 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa mshambuliaji Cristiano Ronaldo katika maisha yake ya soka na anastahili kupata tuzo ambazo amekuwa akishinda kila kukicha.
Mchezaji huyo bora wa dunia kwa mara nne, usiku wa Jumatatu hii alishinda tuzo nyingine ya mchezaji bora wa dunia ya FIFA na kuwabwaga wapinzani wake Lionel Messi wa Barcelona na Antoine Griezmann wa Atletico Madrid.
Ronaldo ameshindwa kuzuia furaha yake na kuamua kuweka wazi sababu ya kushinda tuzo hizo kupitia mtandao wa Twitter aliandika, “You don’t lift the trophy for best player in the world without your team. #JustDoIt.”
“Delighted to win The Best FIFA award. Wouldn’t be possible without my teammates, coaches and you who support me every day. Thanks everyone!,” ameandika katika Picha nyingine aliyoiweka katika mtandao huo.
Hii ni tuzo ya pili kubwa kushinda Ronaldo baada ya Ballon d’Or aliyoshinda mwezi Disemba kutokana na kufanya vizuri msimu uliopita.
Klabu ya Azam FC imemshusha kocha mpya anaejulikana kwa jina la Aristica Cioaba kutoka Romania.

Kocha huyo amepewa mkataba wa miezi sita kwa ajili ya matazamio kama atafanya vizuri huenda akapewa mkataba wa muda mrefu lakini kinyume na hapo atafata nyayo za akina Zeben Hernandez.
Afisa habari wa Azam FC Jafar Idd amesema Aristica Cioaba atasaidiwa na makocha wazalendo ambao wanaiongoza Azam kwa sasa wakiongozwa na Idd Cheche.
“Tumeshapata kocha mpya kutoka Romania ambaye tumempa mkataba wa miezi sita ili tuweze kuangalia uwezo wake. Kama atafanya vizuri basi tunaweza kumuongezea muda,” anasema Jafar Idd uku akiziua tetesi za makocha wazawa kujiunga na Azam.
“Kwa sasa atakuwa akisaidiwa na makocha wetu wazalendo ambao wapo na timu wakiongozwa na Idd Cheche.”
Baada ya Zeben na wasaidizi wake kutimuliwa, ziliibuka tetesi kuwa huenda Karl Ongala ambaye aliwahi kuitumikia klabu hiyo akiwa mchezaji na kocha msaidizi akarejeshwa kwenye benchi la ufundi la Azam FC.
Mkwasa pia ni miongoni mwa makocha waliotajwa kupewa jukumu la kuinoa Azam baada ya kuachana na timu ya taifa ya Tanzania lakini ujio wa Aristica Cioaba unamaliza tetesi hizo.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kiliamua kumchukua aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, ajiunge na chama hicho baada ya kubaini katika utafiti maalum uliofanywa na shirika moja kutoka nchi za nje kwamba alikuwa na uwezo wa kubeba asilimia 18 ya kura zote katika uchaguzi mkuu kuliko mgombea mwingine wa urais katika uchaguzi mkuu uliopita.
Hayo yalizungumzwa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, wakati akihojiwa na Global TV Online ambapo alisema pia Lowassa aliongoza wagombea wote katika utafiti huo.
“Wazungu wakatuambia hivi political personalities zote za Tanzania walimfanyia kila mmoja wao walimfanyia uchunguzi wake, wakatuambia hivi ‘katika wote hao ukimweka huyu na huyu, huyu bwana mkubwa Lowassa huyu yeye peke yake anatembea na asilimia 18 ya Tanzania voters,’ aliyekuwa anamfuata alikuwa na asilimia 11 tu. Kwahiyo Lowassa as Lowassa alikuwa na eighteen percent ya likeability ya kupendwa na hao Watanzania akienda huku anaenda na asilimia 18 ya ziada, akienda huku anaenda na asilimia 18 za ziada nyingine ongezeeni,” alisema Lissu.
“Tukasema hivi, ‘tunataka kushinda uchaguzi eeh tuzungumze na Lowassa’ na Dkt Slaa akasema tuzungumze na Lowassa tukamwambia ‘Dkt una mawasiliano naye’ akasema ‘sina mawasiliano naye, ila kuna mtu ambaye anaweza akawezesha mawasiliano naye ni nani? Askofu Gwajima’ tunaelewana, so this how we got Edward Lowassa.”
Shirikisho la Soka Duniani FIFA hatimaye limepitisha mabadiliko ambapo kuanzia mwaka 2016 timu zitakazoshiriki Kombe la Dunia zitaongezeka kutoka 32 hadi kufikia 48.
Mpango huo ulipitishwa katika mkutano mkuu nchini Uswizi kwa kupigia kura mpango wa kupanua Kombe la Dunia liwe linashirikisha mataifa 48 huku mabara ya Afrika na Asia yakitarajia kunufaika zaidi.
Baada ya mabadiliko hayo, kuanzia katika mashindano ya mwaka 2026, kutakuwa na makundi matatu yenye timu 16 kila moja.
Mpango huo ambao umekuwa ukipigiwa debe na Rais wa shirikisho hilo Gianni Infantino.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemteua mwanawe Meja Jenerali Muhoozi Kainerugaba, kuwa mshauri mkuu wa rais kuhusu operesheni maalum.



Mke wa Museveni, Bi Janet Kataaha Museveni ni Waziri wa Elimu na Michezo, wadhifa ambao alikabidhiwa Juni mwaka jana.
Jenerali Kainerugaba amekuwa kamanda wa kikosi maalum cha wanajeshi (SFC) chenye jukumu la kutekeleza operesheni maalum za kijeshi.
Kikosi hicho husimamia ulinzi wa rais na kulinda maeneo muhimu kwa serikali Uganda.
Luteni kanali Don Nabaasa amepandishwa cheo na kuwa kanali na akateuliwa kaimu kamanda wa SFC.
Rais Museveni pia amemteua mkuu mpya wa majeshi, Meja Jenerali David Muhoozi ambaye amepandishwa cheo na kuwa jenerali.
Mkuu wa majeshi wa awali, Jenerali Edward Katumba Wamala amehamishwa na kuteuliwa waziri wa ujenzi.
Msanii mkongwe katika muziki wa Bongo Flava, Ruta Bushoke amefunguka ni mipango gani ambayo yeye binafsi amejipangia kwa mwaka huu wa 2017.
Bushoke amesema mwaka huu amejipanga zaidi katika kazi zake za muziki na kujikita kwenye biashara ya kilimo na ufugaji kwani hiyo ilikuwa ni ndoto yake ya muda mrefu lakini time hii ameamua kuichukulia serious.
“Nimepanga niwe mkulima na mfugaji ambaye mwisho wa siku naweza kujivunia pia part nyingine ya kazi ambayo naifanya,” amesema. “Nataka niwe mkulima na mfugaji, 2017 nataka mwaka niwe hivyo Mungu anipe tu uzima,” ameongeza.
Kuhusu muziki, muimbaji huyo amesema, “2017 nataka niwape mashabiki wangu muziki mzuri, najua wamemiss sana kusikia kazi zangu kama sasa hivi nina kazi ambayo inafanya vizuri ambayo nimemshirikisha Maua Sama inaitwa ‘Tupendane Sasa’ na bado kuna kazi nzuri nimeshafanya watazisikia.”
Unywaji wa pombe uliopitiliza huongeza hatari ya kupata homa ya ini (Athari mbaya za dawa kwa ini) pale unapotumia dawa aina ya Acetaminophen maarufu kama Paracetamol au Panadol.
Hii ni kwa sababu unywaji wa pombe hupunguza akiba ya “Glutathione” mwilini kemikali inayolinda chembe hai za ini. Ili acetaminophen itolewe mwilini haina budi kuvunjwa vunjwa na ini ilikupata kemikali ambayo itatolewa mwilini kupitia mkojo pale utakapokojoa.
Moja wapo ya zao la kuvunjwa vunjwa kwa acetaminophen ni N-acetylbenzoiminoquinone ambayo inatakiwa kuungana na Glutathione lasivyo itaungana na seli /chembe hai za ini na kuziharibu na kupelekea homa ya ini.
Hivyo basi kupungua kwa Glutathione mwilini kutokana na unywaji wa pombe kutaifanya kemikali hii hatari ipate nafasi ya kuungana na chembe hai za kwenye ini na kusababisha madhara.
Ikumbukwe kwamba unywaji wa pombe uliopitiliza peke yake ni hatari kwa afya ya ini lako, kwa hiyo unapochanganya na matumizi ya paracetamol hatari kwa ini huongezeka maradufu.
Peter Urio, Paul J Kirutu pamoja Abdillah Mnenge ambao pia ni wataalam waliobobea katika maswala ya dawa, vipodozi na utafiti wamesema sio lazima mtu ajioverdose kupata madhara yatokanayo na unywaji wa pombe na acetaminophen, hata katika dozi ya kawaida mtu anaweza kupata madhara makubwa ya kupata homa ya ini endapo atatumia pombe na paracetamol kwa wakati mmoja.
Nitoe wito kwa wanywaji wa pombe kupita kiasi kufikiria mara mbili mbili juu ya afya zao na maisha yao kwa ujumla.
Your Health, My Concern
BY FORD A. CHISANZA
Intern pharmacist
Tanzania Food And Drug Authority (TFDA)
Location: Off Mandela Road, Mabibo – External,
P.o.Box: 77150, Dar Es Salaam, Tanzania.
Mobile:+255 652466430/+255 684363584
Email: fordchisanza@gmail.com
fordchisanza@yahoo.com
Moja kati ya tamaduni na desturi za Kiafrika ni kuamini katika wafu. Watu wa jamii nyingi za kiafrika wanaishi katika dunia hii. Inaaminika mtu akifa ana uwezo wa kukupa baraka na laana, hivyo si ajabu kuona makabila mbalimbali kwenda makaburini kupata baraka au kuondoa laana baada ya mambo kwenda ndivyo sivyo.
Alfajiri ya tarehe 7/04/2012 gwiji wa filamu za bongo movie marehemu Steven Kanumba aliaga dunia! Tarehe 07/04 atatimiza miaka mitano tangu apate pumziko lake la milele. Hakuna ambaye hajui achilia mbali kipaji chake maridhawa lakini juhudi na kujituma kwa icon huyu wa bongo movie. Alifanya kila aliloweza kuhakikisha tasnia ya filamu inafikia kule walipo wenzetu waliopiga hatua katika tasnia hiyo – Kanumba ameondoka na kafa na bongo movie!
Baada ya Kanumba kufariki, waliibuka watabiri mbalimbali waliotabiri kuwa hicho ndio kilikuwa kifo cha bongo movie. Pengine waliona mbele na wana kila sababu ya kuonekana ni watabiri haswa kwani lile walilotabiri ndiyo tunalishuhudia sasa!
Hakuna jipya linaloendelea kwa sasa kwenye kiwanda cha bongo movie. Kila kukicha image mbaya juu yao inaongezeka kuliko idadi ya scenes, skendo ndo zimezidi kuliko kazi wanazofanya. Kiukweli inahuzunisha na kusononesha sana.
Inahuzunisha hasa ukikumbuka kuwa pengine Uncle JJ angekuwepo tusingekua hapa. Wakati huu ambao idadi ya mitandao ya kijamii na watumiaji wake hapa nchini imekuwa kubwa, naamini hii ingekuwa fursa adhimu kwa Steven ambaye kila uchwao alikuwa akitafuta fursa ya kuhakikisha kazi zake zinapenya na kuwafikia watu wengi zaidi. Dada zangu na kaka zangu wa bongo movie wao wanaitumia mitandao hiyo kuonyesha mavazi na mali wanazomiliki, kutupa na kujibu madongo na siku hizi kuweka matangazo uchwara!
Kwa wote mnaohusika kwenye kiwanda bongo movie, sasa mna kila sababu ya kujisikia aibu kwa watu kumkumbuka marehemu eti kwa kitu ambacho mngeweza kufanya tena pengine kwa ufanisi mkubwa kulinganisha na yeye. Lakini badala yake nyie kwa nyie mnachukiana, mnaoneana wivu usio na maana na mmejaa majungu(hii ni kwa mujibu wenu wenyewe mmesikika mkisema) au mnasubiri siku ya kuadhimisha kifo chake mkatambike?
Kila nikiangalia naona kuna fursa kwa nyie kuamka tena na kuliteka soko la ndani na Afrika kwa ujumla, mna haiba, mvuto, vipaji vya kuweza kufanya hivyo. Najua na natambua changamoto mnayoipata katika wizi wa kazi na maslahi mnayopata lakini hamuwezi kukaa tu mkilalamika pasi kuungana. Kuweni wabunifu katika kazi zenu, mkianza kuwekeza nguvu katika kufanya yaliyo bora ni rahisi kutatua changamoto mlizonazo.
Brothers and sisters LuLu, Wema, Kajala, Uwoya, JB, Gabo, Richie na wengine, msione kawaida kuona mitaani kazi za Kihindi na Kinijeria zilizotafsiriwa zikitazamwa kwa wingi kuliko movies za kitanzania. Wabongo wanapenda kazi zenu wanaangalia hizi kwa kuwa sokoni hakuna kazi zenu na zilizopo hazina ubora wa hadithi, picha, sauti na uigizaji pia.
Mwaka huu uwe wa mabadiliko kwenu, oneni wivu kuona nyie ndo mnafanya kazi ya kupromote kazi za Bongo Flava na Bongo Flava hawana cha kusapoti kutoka kwenu. 2017 uwe mwaka wa mabadiliko kwenu na tuone mkiliteka soko kwa mara nyingine.
Waziri mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa serikali ya Tanzania itaendeleza ushirikiano wake na nchi ya China, katika nyanja mbalimbali ikiwemo sekta ya viwanda, nishati na miundombinu kupitia uwekezaji.
Waziri Majaliwa ametoa kauli hiyo Jumatatu hii jijini Dar es Salaam, wakati wa mazungumzo yake na waziri wa mambo ya nje wa China, Wang Yi kwa niaba ya Rais Dkt John Magufuli ambapo amesema Tanzania ipo tayari kupokea makampuni kutoka China kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali nchini.
“Tanzania iko tayari kupokea kampuni zaidi za China kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali nchini.Tupo tayari kupokea viwanda kati ya katika kipindi cha miaka mitatu ijayo,” amesema.
Kwa upande wake, Wang amepongeza utendaji kazi wa Rais Magufuli pamoja na viongozi wengine hususan katika mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi na tayari matunda yameanza kuonekana.
“Serikali ya China kwa sasa iko katika mkakati wa kuhamishia viwanda vyake vingi barani Afrika. Iliamua kuichagua Tanzania kuwa moja katika ya nchi watakayohamishia viwanda hivyo kutokana na kuridhishwa na dhamira inayoonyeshwa na serikali katika kuleta maendeleo,” alisema Wang.
Waziri Wang, yupo nchini kikazi kwa ziara ya siku moja ya kikazi hivyo anatarajiwa kuondoka hii leo.
Rapper Young Killer anadai kuwa wimbo wake mpya, Sinaga Swaga umekuja kuirudisha ‘real hip hop’ kwenye mstari.
Amedai kuwa kipindi cha hivi karibuni rappers wengi wa Bongo wamekuwa wakilegeza ngoma zao ili kuvutia biashara, lakini yeye ameamua kukaza.
“Dhumuni la kufanya hii ngoma, nimetaka kuwaonesha kwamba hip hop yetu bado ipo na ina nguvu kubwa na ina uwezo wa kufika mbali zaidi ya hapo ambapo ipo endapo tutaendelea kuisupport na kuipa nafasi,” rapper huyo amemuambia mtangazaji wa Pride FM, Eddy Msafi.
Rapper huyo amesisitiza kuwa masikio ya mashabiki wa muziki Tanzania yanahitaji ngoma za aina ya Sinaga Swaga na si kupewa nyimbo za kuimba na kuchezeka tu.

Nusu fainali ya kombe la Mapinduzi yanayo fanyika mjini Zanzibar, itafanyika leo kati ya mchezo wa wapinzani wa jadi Simba na Yanga unaotarajiwa kufanyika leo katika uwanja wa Aman majira saa mbili na robo usiku.
Mchezo huo unao subiriwa kwa hamu na wadau wengi wa soka utakuwa wa kwanza kwao kukutana kwa mwaka 2017 kwenye kombe la Mapinduzi.
Timu ya Yanga wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na majeruhi baada ya kupata kipigo cha magoli 4 kwa bila dhidi ya Azam, wakati Simba wao wakiwa na rekodi nzuri kwenye mashindano hayo wakiwa hawaja poteza mchezo hata mmoja.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeendelea na mpango mkakati wake wa kuhakikisha inatoa elimu ya kodi na inamfikia kila mdau ili kuwajengea uelewa wa masuala ya kodi na uhiyari wa kuilipa.


Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Diana Masala
Hivi karibuni mamlaka hiyo ilikutana na wasanii mbalimbali wa maigizo na muziki ili kuwafundisha kuhusu masuala mbalimbali ya kodi pamoja na umuhimu wa kulip
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Diana Masala, anasema kila msanii mwenye sifa za kulipa kodi anatakiwa kulipa na kwamba huduma nzuri zinazotolewa na Serikali zitatumiwa na kila Mtanzania bila kubagua.
Katika semina na wasanii hao, TRA iliwafundisha kuhusu Kodi ya Mapato pamoja na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na kwamba kila mtu mwenye kipato anatakiwa kulipa kodi kwa mujibu wa sheria za nchi.
Sambamba na kuwapa elimu ya kodi, pia ilipokea maoni mbalimbali kutoka kwa wasanii hao ili kuweza kujua changamoto wanazokabiliana nazo waweze kuzitatua ikiwa ni pamoja na kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanya kazi zao zitakazowapatia kipato ambacho watatakiwa kukitumia kulipia kodi.
Pia alisema wasanii wote ambao hawajajisajili wanatakiwa kuhakikisha wanajisajili katika ofisi za TRA kupatiwa Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi (TIN) na baadaye atakadiriwa kodi anayostahili kulipa kulingana na namna anavyopata mapato yake.
Kila msanii ambaye mauzo ghafi yake hayafikii milioni 20 kwa mwaka atahesabika kama mlipa kodi mdogo ambaye atakadiriwa kodi kulingana na mauzo yake au faida aliyoipata.

Masicka linked with Shawn Dan Productions on this gritty new gangsta anthem “Born Criminal.” The track was previously leaked only as a rough mix but the producers decided to master it and drop it as the first new joint from the fast rising deejay for the new year.
Last year we heard a lot from Masicka including collaborations with Bounty Killer and Ishawna. Seems this year he is already prepping his fans for a busy year. The dancehall young gun is also working on his debut project due sometime this year. “Drop in a dust / them feel a Christmas a come when man tell them barrel a buss / Boy forehead a crush, Every rassclat shot out a the maggi a rush,” Masicka deejay over a 1990s feel rap beat.
Stream Masicka new single “Born Criminal” below.


Masicka linked with Shawn Dan Productions on this gritty new gangsta anthem “Born Criminal.” The track was previously leaked only as a rough mix but the producers decided to master it and drop it as the first new joint from the fast rising deejay for the new year.
Last year we heard a lot from Masicka including collaborations with Bounty Killer and Ishawna. Seems this year he is already prepping his fans for a busy year. The dancehall young gun is also working on his debut project due sometime this year. “Drop in a dust / them feel a Christmas a come when man tell them barrel a buss / Boy forehead a crush, Every rassclat shot out a the maggi a rush,” Masicka deejay over a 1990s feel rap beat.
Stream Masicka new single “Born Criminal” below.
 Vybz Kartel

Vybz Kartel is celebrating his 41st birthday today and some of dancehall top acts are helping him to mark the milestone.
Kartel, who is currently in prison for a murder wrap, was born on January 7, 1976 in Kingston but grew up in Waterford, Portmore. The deejay, whose real name is Adidja Palmer, started his career as a teenager back in the early 1990s under the name Adi Banton. His debut single “Love Fat Woman” was voiced under the One Heart Label owned by Alvin Reid. In the mid to late 90s he joined a group called Vybz Cartel but that group was short-lived.
Vybz Kartel big break in dancehall came in early 2000s when he joined the Bounty Killer lead Alliance. He released a slew hit songs including a full length album “Up 2 Di Time” which won him a ton of new fans. From there he went on to become a household name in the genre, but a 2011 murder charge prove to be his biggest test to date. Despite his subsequent conviction and life sentence, Vybz Kartel manages to remained one of the most relevant artists in dancehall over the past five years.
Today several dancehall artists including Konshens, Popcaan, NotNice, Tommy Lee Sparta, Jah Vinci, Masicka, and many more.
“Iconic. Blessed earthstrong. @vybzkartel #capricornrule,” Konshens said.

“Big up pan yu earth strong general neva drop respect or ratings for you yet and neva will more life @vybzkartel NEVER UNGRATEFUL OR ACT LIKE MI NUH KNOW WEH YU DO FI ME ALWAYS AND FOREVER GREATFUL #WORLDBOSS #GAZA #EMPIRE #kingofdancehall,” Jah Vinci wrote.

“Big up the gaza don pan him strong. Portmore have the baddest artist dem. Physically/musically,” Masicka wrote.


Vybz Kartel promises a thousand new songs this year and “Hold It” is the first of the batch. The track was produced by Studio Vibes Productions and distributed by 21st Hapilos.
Kartel is celebrating his 41st birthday today in prison and a ton of dancehall entertainers are sending their well wishes. “Don’t hang your hat where you can’t reach it / Well if yo can’t buy oxtail hold a chicken back steak / Nobody no badder than gas pain / But my youth gwaan hold it,” Kartel deejay. This song will sure reignite rumors that the deejay is recording music in prison. The allegation was a big part of the reason for his sudden prison transfer back in November from Horizon Remand to Tower Street.
Listen to Vybz Kartel new song “Hold It” below.



Reggae artist Jae Prynse poise to do great thing in 2017.
The artist has been endorsed by the general Bounty Killer along with Taurus Riley. Jae Prynse has been on the music sense since 2013. He is signed to United Kingdom based live MB Music. Not only is the upcoming artist getting recognition locally but also internationally, especially with his latest single released last August “Try Harder” produced by Frens For Real Recording. The single is played on radio in countries such as UK, US, Switzerland and Germany and locally on Irie, Zip FM and Sun City radio stations.
Some of his other singles include: “Fi Mama”, “Who Feels It Knows It”, “Good Living”, “Faker”, “It Coulda Be Worse” and “Serenity”.
Jae Prynse whose real name is Prince Williams grew up in Love Lane in Downtown Kingston. Jae turned to music for healing when his brother was murdered in 2009 who was an aspiring artist (True Man Chew Stick). “I used music to escape from the negatives that surrounded me” he said.
In 2016, Jay toured UK alongside reggae superstars Luciano and Jah Bouks. He performed in places such as London, Birmingham and Ipswitch. Locally, Jay was featured on GT Taylor Christmas Extravaganza where he performed with a bang.
The on-the-rise artist bases his conscious lyrics on his own personal experiences. He regarded 2016 as a fantastic year and hopes to have a better 2017.


Sizzla Kalonji kick in off the new year with some fresh music. The reggae/dancehall legend new single “Buss It” is gaining a lot of traction on social media.
The single is featured on the 8806 Riddim, a production from Stampede Music and distributed by Zojak. Been a while since we’ve heard some new music from Sizzla but he has a habbit of just dropping a new album without notice. Sizzla is hot off a number of big performances over the holiday including a well received set at GT Extravaganza.
Listen to Sizzla single “Buss It” below.

Cassidy ni mnyama kwenye kipaza. Na kwa freestyle tu, ni mmoja wa rappers wanaozipiga haswaaa. Hivi karibuni kwenye show ya Dj Whoo Kid, rapper huyo toka Philadelphia, akiwa na producer wake wa zamani, Swizz Beatz alikinukisha mbaya. Mtazame hapo chini.
Msanii wa Kundi la Navy Kenzo, Aika ameonyeshwa kusikitishwa na kuvunjwa moyo na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakizivujisha nyimbo kutoka kwenye albamu yao mpya ‘AIM’ na kuzisambaza mitandaoni.
Muimbaji huyo alidai kitendo cha baadhi ya watu hususani bloggers kuchukua nyimbo hizo kwenye albumu na kuziweka mitandaoni kinakuwa kinawavunja moyo kwani kinasababisha biashara yao kupunguza kasi na kuharibu mauzo ya album hiyo mtaani.
“Inasikitisha sana pale msanii unapofanya kitu kikubwa halafu baadaye mtu anaitoa bure kazi yako, sisi kama Navy Kenzo tumefanya kazi kubwa sana mpaka kukamilisha hiyo kazi, tumethubutu, sasa unapoona blogs zinaweka zinatuharibia biashara hata watu wanaonunua albamu wakiona tena mtandaoni wanajisikiaje,” Aika alikiambia kipindi cha EA Radio.
Muimbaji huyo alisisitiza kuwa anatambua bloggers huenda wanajua wana wa’support’ kwa ku-upload nyimbo hizo kwenye mitandao ya jamii ili kusaidia albumu kuuzika lakini huenda wengine hawajui kile wanachofanya kinawaharibia wao soko la albumu yao mtaani.
Chama cha wafanyakazi wa Serikali za mitaa (TALGWU)kimewatata viongozi wa kisiasa kuacha udhalilishaji kwa watendaji ngazi za kata,vijiji na mitaa.
Akizungumza na waandishi wa habari,Katibu mkuu wa chama hicho, Rashid Mtima alisema tayari wameshapeleka barua kwa makatibu tawala kwa lengo la kukusanya matukio hayo ya udhalilishaji.
“Kwa mfano tunakumbuka lile tukio la afisa ardhi aliyedhalilishwa na Makonda hivi karibuni, basi huko kwenye halmashauri, watendaji wa serikali za mitaa wananyanyasika sana,” alisema Mtima.
“Akikosea achukuliwe hatua lakini ni vyema akiachwa akajieleza, zipo taratibu za kufuata na sio kufuata umaarufu kwa njia hizo, tunaamini njia ya mazungumzo ndiyo njia sahihi tunaamini hali kama hiyo haitajitokeza tena”.