Kasi ya wanachama wa CCM kutangaza nia ya Kugombania
Nafasi ya Urais imezidi kuendelea ambapo leo Aliyekuwa waziri mkuu wa awamu ya
tatu Mh Fredrick Sumaye ametangaza nia yake ya kuwania nafasi hiyo katika Uchaguzi
mkuu wa Mwaka huu.
WAZARI MKUU MSTAAFU SUMAYE
Akitangaza nia yake mbele ya waandishi wa habari na
wanachama wa chama cha Mapinduzi katika ukumbi wa Hyatt Regency Kilimanjaro
Hotel Sumaye ametaja vipaumbele vyake kuwa ni Kukuza Uchumi,Kuboresha huduma za
kijamii pamoja na kupambana na maovu ikiwemo Rushwa,ufisadi na Biashara ya
madawa ya kulevya.
Sumaye amesema kuwa amejiandaa kwa dhati kupokea
kijiti atakachokiacha Rais wa sasa Mh Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuwa amejipima
na kuona anajitosheleza kuwatumikia watanzania kwa awamu ya tano ya urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kuhusu kukuza uchumi Mh Sumaye amesema kuwa eneo kubwa
linalohitaji msukumo ni kilimo kwa kuboresha mbegu bora na masoko sambamba na
kusimamia viwanda vya ndani.
Sambamba na hayo Mh Sumaye amesema kuwa kuhusu
kupambana na maovu ataunda chombo na mahakama maalumu ya kushughulikia
Rushwa,Ufisadi,Uhujumu uchumi na biashaya ya Madawa ya kulevya.
Akizungumzia sifa za Rais ajaye Sumaye amesema kuwa
anatakiwa awe mtu aliye tayari Kujitafakari na kujipima
kiakili,Kiafya,kimaadili na kidhamira kwa maendeleo ya Taifa na si ya familia
na binafsi.
Mh Fredrick Sumaye amekuwa kiongozi wa saba wa chama
cha mapinduzi kutangaza nia ya kugombea nafasi ya urais baada ya Mh Edward
Lowassa,Steven Wasirra,Mwigulu Nchemba,Mark Mwandosya na Ally Karume kutangaza
nia hiyo.
0 maoni:
Post a Comment